Mwanadada anaye tamba katika tasnia ya filamu bongo, Aunt Ezekiel
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichozama katika kikao kilichofanyika juzikati, uongozi ambao ulibaki madarakani kundini baada ya Steve kujiuzulu, ulifanya tathmini upya ya memba waliobaki kisha kuwachuja hadi kubaki na wasanii 20 pekee wenye sifa.
“Wamewaengua baadhi ya wasanii ambao
wameona hawana sifa ya kubaki kundini, miongoni mwao ni Devotha, Aunt na
Odama. Wamesema wanahitaji mastaa wenye msimamo siyo kujipendekeza
upande wa Steve, siku si nyingi watayaanika majina ya wenye sifa za
kubaki kundini,” kilisema chanzo hicho.
Staa wa filamu bongo Devota Mbaga.
Baada ya habari hizo kutua katika rada ya
Ijumaa, mapaparazi wetu waliwaendea hewani mastaa hao wakubwa waliodaiwa
kufukuzwa, mambo yalikuwa hivi:
Mkali wa filamu Bongo, Jennifer Kyaka 'Odama'.
Odama: Hakuna kitu kama hicho, wanaoenguliwa ni viongozi siyo wanachama, watanienguaje bila kunipa taarifa? Kwanza ndiyo nasikia sijui chochote ndiyo napata taarifa kutoka kwako.
Kwa upande wa Aunt Ezekiel, simu yake iliita bila kupokelewa.
Post a Comment